sw_tn/psa/029/006.md

844 B

Kauli Unganishi:

Mwandishi anaendelea kuelezea nguvu ya sauti ya Mungu.

Anaifanya Lebanoni kurukaruka kama ndama

Lebanoni inazungumziwa kana kwamba ni ndama mchanga. Hii inasisitiza kwamba Yahwe akizungumza, nguvu ya sauti yake hutikisa ardhi. "Hufanya nchi ya Lebanoni kutikisika kama ndama anaye rukaruka"

kurukaruka

kuruka kidogo hapa na pale

Sirioni kama kama ng'ombe mdogo

Sirioni inazungumziwa kana kwamba ni ng'ombe mchanga. Hii inasisitiza kuwa Yahwe akizungumza, nguvu ya sauti yake hutikisia ardhi. "Huifanya Sirioni kuruka kama ng'ombe mchanga"

Sirioni

Huu ni mlima Lebanoni. Pia unaitwa mlima Hermoni.

Sauti ya Yahwe inatuma miali ya moto

Sehemu zote zenye "sauti" zinamaanisha Yahwe anazungumza. "Yahwe akizungumza husababisha miali ya radi kuonekana angani"

miali ya moto

hii inamaanisha mwale wa radi.