sw_tn/psa/027/009.md

828 B

Usiufiche uso wako kwangu

Uso unawakilisha usikivu wa Yahwe. Msemo "Usiufiche uso wako" ni njia kumwomba Mungu asimkatae. "Usinikatae" au "Usiache kunitunza"

usimgeuza mtumishi wako kwa hasira

Daudi alisema "mtumishi wako" kumaanisha ni yeye mwenywe kwa njia ya unyenyekevu. "usinikasirikie"

usiniache wala kunitupa

Maneno "kuacha" na "kutupa" yana maana sawa. Mwandishi anasisitiza kuwa hataki Mungu amuache.

wala kunitupa

"na usinitupe" au "na usiniache"

Mungu wa wokovu wangu

Nomino dhahania ya "wokovu" inaweza kuelezwa kama "okoa." "Mungu anayeniokoa" au "kwa kuwa wewe ni Mungu unayeniokoa"

Hata kama baba na mama yangu wakiniacha

Hasemi kuwa kweli wamefanya hivi au kwamba watafanya hivi. Wazo lake ni kwamba hata kama wangefanya hivyo, Mungu asingemuacha.

Yahwe atanichukua

"Yahwe atanitunza"