sw_tn/mrk/04/13.md

969 B

Sentensi unganishi

Yesu anaelezea mfano wa udongo kwa wafuasi wake na kisha anawambia kuhusiana na taa kuonyesha vitu vilivyo jificha vitajulikana.

Na akasema kwao

"Na Yesu akasema na wanafunzi wake"

Je hamuelewi mfano huu? Mtawezaje kuelewa mifano mingine ?

Yesu alitumia maswali haya kuonyesha jinsi alivyokuwa na huzuni kwamba wanafunzi wake hawakuweza kuelewa mfano wake. "kama hautaweza kuelewa mfano huu, fikiri jinsi ilivyo ngumu kwa wewe kuelewa mifano mingine"

Mkulima anayepanda mbegu zake

"Mkulima anayepanda mbegu zake huwakilisha"

kwa yule anayepanda neno

"Neno" huwakilisha ujumbe wa Mungu. Kupanda ujumbe huwakilisha kufundisha. "yule anayefundisha watu ujumbe wa Mungu"

Baadhi huanguka kandokando mwa njia

"Baadhi ya watu ni kama mbegu huanguka kandokando mwa njia" au "Baadhi ya watu ni kama njia ya miguu ambapo mbegu huangukia"

njia

"njia ya miguu"

wanapoisikia

Hapa wanapo-"i" sikia urejea "neno" au "ujumbe wa Mungu"