sw_tn/mat/05/21.md

40 lines
1.4 KiB
Markdown

# Sentensi unganishi
Yesu anaendelea kufundisha jinsi alivyokuja kutimiliza sheria za agano la kale. Hapa anaanza kufundisha juu ya kuua na hasira
# Maelezo kwa ujumla
Yesu anawaambia kikundi cha watu juu ya kile ambacho kinaweza kutokea kwao kama watu binafsi. Neno "mme" katika sentensi "mmesikia" na "nawaambia" ni maneno ya wingi. Ile amri ya "usiue"ni ya umoja, lakini unahitaji kuitafsiri katika wingi.
# ilinenwa zamani
Hii inaweza kuelezeka kwa mfumo tendaji. "Mungu alisema na mababu zetu zamani za kale".
# auaye yuko katika hatari ya hukumu
Hapa "hukumu" inamaanisha kuwa hakimu ndiye atakayemhukumu mtu kufa. "Hakimu atamhukumu yeyote amuuaye mtu mwingine"
# kuua ... auaye
Neno hili linamaanisha kitendo cha mauji ya kudhamiria, na wala siyo kila aina ya mauji
# Lakini nawambia
Kiwakilishi "na" kinatia msisitizo. Hii inamaanisha kuwa kile anachosema Yesu kina umuhimu sawa na amri itokayo kwa Mungu. Jaribu kutafsiri hili kataka mazingira yanayonesha msisitizo.
# ndugu
Neno hili linamaanisha muumini mwenzetu
# atakuwa katika hatari ya hukumu
Inaovyoonekana hapa Yesu hamaanishi hakimu wa kibinadamu bali Mungu anamhukumu mtu mwenye hasira kwa ndugu yake.
# mtu usiyefaa ... mjinga
Hii ni mizaha kwa watu wasioweza kufifkiri kwa usahihi. "Mtu asiyefaa" ni sawa na "mtu asiye na akili," ambapo "mjinga" inaongezea wazo la kutokuwa mwaminifu kwa Mungu.
# baraza
Yawezekana hili ni baraza dogo, siyo lile kuu.