sw_tn/mat/05/21.md

1.4 KiB

Sentensi unganishi

Yesu anaendelea kufundisha jinsi alivyokuja kutimiliza sheria za agano la kale. Hapa anaanza kufundisha juu ya kuua na hasira

Maelezo kwa ujumla

Yesu anawaambia kikundi cha watu juu ya kile ambacho kinaweza kutokea kwao kama watu binafsi. Neno "mme" katika sentensi "mmesikia" na "nawaambia" ni maneno ya wingi. Ile amri ya "usiue"ni ya umoja, lakini unahitaji kuitafsiri katika wingi.

ilinenwa zamani

Hii inaweza kuelezeka kwa mfumo tendaji. "Mungu alisema na mababu zetu zamani za kale".

auaye yuko katika hatari ya hukumu

Hapa "hukumu" inamaanisha kuwa hakimu ndiye atakayemhukumu mtu kufa. "Hakimu atamhukumu yeyote amuuaye mtu mwingine"

kuua ... auaye

Neno hili linamaanisha kitendo cha mauji ya kudhamiria, na wala siyo kila aina ya mauji

Lakini nawambia

Kiwakilishi "na" kinatia msisitizo. Hii inamaanisha kuwa kile anachosema Yesu kina umuhimu sawa na amri itokayo kwa Mungu. Jaribu kutafsiri hili kataka mazingira yanayonesha msisitizo.

ndugu

Neno hili linamaanisha muumini mwenzetu

atakuwa katika hatari ya hukumu

Inaovyoonekana hapa Yesu hamaanishi hakimu wa kibinadamu bali Mungu anamhukumu mtu mwenye hasira kwa ndugu yake.

mtu usiyefaa ... mjinga

Hii ni mizaha kwa watu wasioweza kufifkiri kwa usahihi. "Mtu asiyefaa" ni sawa na "mtu asiye na akili," ambapo "mjinga" inaongezea wazo la kutokuwa mwaminifu kwa Mungu.

baraza

Yawezekana hili ni baraza dogo, siyo lile kuu.