sw_tn/mal/01/01.md

934 B

Agizo la neno la Bwana kwa Israel kwa Mkono wa Malaki.

"Bwana alizungumza haya maneno kwa waisrael kupitia Malaki"

Kwa mkono wa Malaki

kupitia kutenda kwa Malaki

Lakini wasema, "Umetupenda kwa namna gani?"

Hili swali linaonyesha shaka, au maswali juu ya ukweli wa neno la Mungu. Mungu anatumia swali kuwakemea watu. Tafsiri mbadala: lakini wasema, "Hujatupenda!"

Hakuwa Esau ndugu yake Yakobo?

"Nitawaambia jinsi ninavyowapenda ninyi. mnajua kwamba Esau ni ndugu yake Yakobo."

Asema Bwana

Bwana mwenye kweli amesema haya"

Nimempenda Yakobo

Bwana alichagua kuwa na mahusiano na Yakobo na kuwa Mungu ya Yakobo.

Nimemchukia Esau

Bwana alimkataa Esau

Nimeifanya Milima yake kuwa ya uharibifu na kuteketezwa

"Nimeifanya milima yake kuwa haifai kukaa ndani yake"

Na nimeufanya urithi wake kuwa sehemu ya mbweha wa mwituni

"Na nimeifanya nchi anayorithi kuwa jangwa ambapo wanyama pekee wanaweza kuishi"