sw_tn/luk/22/31.md

752 B

Taarifa ya kijumla:

Yesu anaongea moja kwa moja na Simoni.

Simon, Simon

Yesu alilisema jina lake mara mbili kuonyesha kwamba kile ambacho alikuwa akiseme kwake kilikuwa cha muhimu sana.

awapate, ili awapepete

Neno "awa" linaonyesha mitume wote.

awapepete kama ngano

Hii inamaanisha kwamba Shetani alitaka kuwajaribu mitume ili kupata makosa.

Lakini nimekuombea

Hapa inamaanisha amemuombea kipekee kabisa SImoni.

kwamba imani yako isishindwe

"kwamba utaendelea kuwa na imani" au "utaendelea kunitegemea mimi"

Baada ya kuwa umerudi tena

"Baada ya kuanza kunifuata tena" au "Baada ya kuanza kunitumikia mimi tena"

ndugu zako

Hii inamaanisha wanafunzi wengine wa Yesu. Tafsiri mbadala: "Waamini wenzako" au "mitume wengine."