forked from WA-Catalog/sw_tn
36 lines
1.3 KiB
Markdown
36 lines
1.3 KiB
Markdown
# kinywa chake kilifunguliwa ... ulimi wake uliwekwa huru
|
|
|
|
Hizi kauli mbili ni maneno picha ambayo pamoja yanasisitiza kwamba Zakaria aliweza kuzungumza ghafla.
|
|
|
|
# kinywa chake kilifunguliwa na ulimi wake uliwekwa huru
|
|
|
|
Kauli hizi zinaweza pia kusemwa katika mtindo wa kutenda. NI: Mungu akafungua kinywa chake na kuuweka huru ulimi."
|
|
|
|
# Hofu ikawajia wote ambao waliishi karibu nao
|
|
|
|
"Wote walioishi karibu na Zakaria na Elizabethi walikuwa na hofu." Walikuwa wamepigwa butwaa kwa njia ya Mungu ya miujiza kumrejeshea Zakaria uwezo wa kuzungumza. NI: "Kila mmoja aliyeishi karibu nao walikuwa katika hofu ya Mungu."
|
|
|
|
# wote ambao waliishi
|
|
|
|
Hii hairejei tu kwa wale majirani wa karibu lakini kwa kila mmoja ambaye aliishi eneo hilo.
|
|
|
|
# wote waliowasikia wao
|
|
|
|
Neno "wao" hapa linarejea kwenye mambo yaliokwisha tokea.
|
|
|
|
# wote waliosikia
|
|
|
|
Hii inarejea kwenye kundi kubwa la watu walioishi Uyahudi yote.
|
|
|
|
# kusema
|
|
|
|
"kuuliza"
|
|
|
|
# Mtoto huyu atakuja kuwa kuwa nani?
|
|
|
|
"Aina gani ya ukuu ambao atakuwa nao mtoto huyu akikua?" Hii pia inawezeakana kwamba swali hili lilikuwa linamaanisha kuwa ni kauli ya kuwashangaza kwa kile walichisikia kuhusu mtoto. NI: "Mtoto huyu atakuwa mkuu wa namna gani!"
|
|
|
|
# mkono wa Bwana ulikuwa pamoja naye
|
|
|
|
Kauli hii "mkono wa Bwana" inarejea nguvu za Mungu. "Nguvu za Mungu zilikuwa pamoja naye" au "Mungu alikuwa anafanya kazi ndani yake kwa nguvu."
|