sw_tn/job/39/19.md

585 B

Maelezo ya jumla

Yahweh anaendelea kumtia changamoto Ayubu

Je umempa farasi ... panzi?

Yahweh anatumia maswali haya kutia mkazo kwamba ni yeye ndiye huyafanya mambo haya ambayo Ayubu hayawezi.

umeivika shingo yake

Neno 'kuvika" ni njia ya kuelezea jinsi ambavyo Yahweh alivyoifanya shingo ya farasi.

manyoya yake

ni nywele ndefu ambazo hushuka chini kutoka katika shingo ya farasi na hutisika wakati farasi anapoondoka.

nzige

ni aina kubwa ya panzi ambayo yaweza kuruka kwenda mbali na kwa haraka sana.

mlio

ni sauti kubwa ambayo farasi huitoa katika pua zao.