sw_tn/job/29/14.md

845 B

Nilivaa haki, nayo ikanifunika

watu wa wakati ule waliongelea haki kama vazi. KTN: "Nilitenda haki, nayo ikawa kama vazi la kujisitiri juu yangu"

uadilifu wangu ulikuwa kama joho na kilemba

watu wa wakati ule waliongelea uadilifu kama vazi. KTN: "Nilitenda kwa adili, na ilikuwa kama joho na kilemba juu yangu"

kilemba

vazi refu ambalo wanaume hufunga kuzunguka vichwa vyao, huvaa kama kofia.

nilikuwa macho kwa watu vipofu

Hii inamaanisha kuwasaidia watu vipofu. KTN: "nilikuwa kama macho kwa ajili ya watu vipofu" au "niliwaongoza watu vipofu"

nilikuwa miguu kwa watu viwete

"nilikuwa kama miguu kwa watu viwete" au "niliwasaidia watu viwete"

nilikuwa baba kwa watu wahitaji

hapa neno baba linawakilisha kutoa kwa ajili ya watu. KTN: "Nilitoa kwa ajili ya watu wahitaji kama baba anavyotoa kwa ajili ya watoto wake"