sw_tn/job/28/12.md

1.1 KiB

Maelezo ya Jumla

kwenye 28:12-28, hekima na maarifa vimesemwa kama vitu ambavyo vipo mahali fulani na watu wanataka wavipate. kutafuta hekima na maarifa inawakilisha kuwa na busara na kujifunza kufahamu vitu kwa uzuri.

Je hekima itapatikana wapi? Je ni sehemu gani yenye maarifa?

Maswali haya yanamaana moja na yametumika kuonesha kuwa ni vigumu kupata hekima na maarifa.

Je hekima itapatikana wapi? Je ni sehemu gani yenye maarifa

Kuwa mwenye hekima na maarifa inazungumziwa kana kwamba ni kutafuta hekima ana maarifa: KTN: "Jinsi gani watu huwa na hekima? Jinsi gani watu hujifunza kufahamu vitu kwa uzuri?"

Binadamu hajui thamani yake

Hapa inaweza kumaanisha kuwa:- 1) "Watu hawajui uzuri wake" au 2) "Watu hawajui mahali ilipo"

wala haipatikani katika nchi ya walio hai

nchi ya walio hai inamaana ya ulimwengu huu ambapo watu wanaishi. KTN: "na hakuna mtu anayeweza kupata hekima katika ulimwengu huu "

Maji yenye kina... yanasema, 'haiapo ndani kwangu' bahari inasema, ' haipo kwangu'

vilindi vya maji na na bahari vinasimama kama watu wanaoweza kuongea. KTN: "Hekima haipo ndani ya vilindi vya maji chini ya ardhi, wala katika bahari"