sw_tn/job/21/31.md

1.1 KiB

Sentensi Unganishi

Ayubu anaendelea kuzungumza kwa rafiki zake.

Ni nani ataishutumu njia ya mtu mwovu kwenye uso wake?

Ayubu anatumia swali hili kupinga dhana ya kuwa waovu mara zote hupatwa na hukumu. KTN: ' Hakuna anayemshutumu mtu mwovu kwenye uso wake"

kwenye uso wake

Hapa inamaana kuwa hakuna mtu atakaye kwenda moja kwa moja kwake na kumshutumu.

Ni nani atamlipiza kwa yale aliyotenda?

Ayubu anatumia swali hili kupinga imani ya rafiki zake kuwa waovu mara zote hupatwa na hukumu. KTN: ' Hakuna mtu anayemlipiza mwovu kwa mambo mabaya aliyotenda"

atazikwa

KTN: " Watu watambeba"

Madonge ya bondeni yatakuwa matamu kwake

Maana yake ni kwamba mtu mwovu atakuwa na kifo chema na maziko mema baada ya kutimiza maisha yake. KTN: "atafurahia kufukiwa kwa uchafu wa bondeni" au " atafurahia kuzikwa katika uchafu wa bonde"

watu wote watamfuata, kutakuwa na watu wengi mbele yake

Ayubu anaweka makazo kuwa kundi kubwa la watu watakuwepo katika harakati za mazishi yake kutoa heshima. KTN: "idadi kubwa ya watu watakwenda kwenye eneo la makaburi; baadhi wakiwa mbele na wengine nyuma"