sw_tn/job/14/01.md

1.3 KiB

Habari za Jumla:

Sura hii ni mwendelezo wa hotuba ya Ayubu, iliyoanza 12:1. Ayubu anazungumza kwa Mungu.

Mwanadamu, ambaye amezaliwa na mwanamke,

Sentensi hii ina maanisha watu wote,wanaume na wanawake wote wamezaliwa katika ulimwengu huu.

huishi siku chache tu

hapa imetumika lugha ya kukuza jambo ili kutoa msisitizo kwamba watu huishi muda mfupi tu. " hushi muda mfupi sana"

amejaa mahangaiko.

Kujaaa "mahangaiko" inaonyesha kupata mateso mengi. "yeye ana mahangaiko mengi" au " anateseka sana"

Yeye huchanua kutoka katika ardhi kama ua na kukatwa chini;

Kama maisha ya ua, maisha ya mtu ni mafupi na ni rahisi kuuawa.

yeye hukimbia kama kivuli na hawezi kudumu.

Maisha mafupi ya mwanadamu yamelinganishwa na kivuli ambacho hutoweka haraka.

Je, wewe unatazama chochote katika hivi?

Ayubu ana maanisha kuwa yeye hahitaji Mungu amsikilize sana." Wewe hautazami chochote haya" au " Wewe haunisikilizi sana mimi "

tazama katika hivi

Kumtazama mtu kunawakilisha kuwa makini kumsikiliza ili kumhukumu yeye. "Kuwa tayari kusikiliza" au " tazama makosa ndani yake"

Mnanileta mimi hukumuni pamoja nanyi?

Ayubu anatumia swali hili kuonyesha kushangaa kwake kuwa Mungu anamhukumu yeye ingawa Ayubu si wa thamani kama ua."Lakini wewe wanihukumu mimi"