sw_tn/job/06/07.md

788 B

Habari ya Jumla:

Mwandishi anaendelea kutumia ulinganishaji katika kila mistari hii, kuwasilisha wazo moja akitumia maelezo mawili tofauti kusisitiza mateso yake makali sana na haja yake ya kufa.

Nakataa kuvigusa

"Wao" inahusu chakula chenye ladha mbaya. Hapa Ayubu anaendelea kutumia sura ya chakula kibaya kama sitiari kwa hali ya mambo yasiyokubalika.

Oo, kama nigeweza kupata haja yangu; oo, kama Mungu angeridhia jambo nilitamanilo sana

"Oo kwamba Mungu angefanya kile ambacho nimemwomba yeye kufanya"

kama Mungu ingempendeza kuniangamiza mara moja

"Kwamba Mungu angelisonga mbele na kuniangamiza mimi"

kwamba angeulegeza mkono wake na kuyakatilia mbali maisha yangu

"kwamba angelitenda haraka na kufupisha maisha yangu"

angeulegeza mkono wake

"tenda haraka"