sw_tn/job/03/17.md

791 B

Habari za Jumla:

Ayubu anabadilisha mazungumzo yake kutoka kufa mpaka uzima baada ya kifo.

Huko waovu huacha kusumbua; huko waliochoka hupumzika.

Ayubu anatumia usambamba kusisitiza kuwa wanyonge watapata pumziko kutoka kwa wale walio wasababishia magumu.

Huko waovu huacha kusumbua

Ayubu anaongea kuhusu sehemu ambayo watu huenda baada ya wao kuacha kuishi. "Katika sehemu hiyo, watu waovu huacha kusumbua"

sauti ya msimamizi wa watumwa

Hapa "sauti" ni mfano wa nguvu ambayo msimamizi wa watumwa anakuwa nayo juu ya watumwa. "Hawako tena chini ya udhibiti wa watumwa"

wadogo na watu maarufu

Hii ni tamathali ya usemi ambayo humaanisha "watu wote, watu masikini na watu matajiri."

mtumishi yuko huru kwa bwana wake huko.

Mtumishi hana wajibu wa kumtumikia bwana wake.