sw_tn/job/01/06.md

1.2 KiB

siku ambayo

Hii haikuwa siku maalumu. Kusanyiko lilifanyika mara kwa mara. "wakati ambapo" au "siku moja wakati"

watoto wa Mungu

Hii inamaanisha malaika, viumbe wa mbinguni.

kujihudhurisha mbele za BWANA

"kusimama pamoja mbele za BWANA kama alivyo waagiza kufanya"

Natoka kuzunguka zunguka duniani, kutembea huku na huko humo

Msemo "kuzunguka zunguka" na "kutembea huku na huko" inakusudia kazi moja ya kusisitiza ukamilifu wake. "Kutoka mahali popote duniani."

BWANA

Hili ni jina la Mungu ambalo alilifunua kwa watu wake katika Agano la Kale. Tazama ukurasa wa tafsiri ya Neno Yahweh kuhusu namna ya kulitafsiri

kutembea huku na huko humo

"huku na huko" inahusian na kusafiri juu ya dunia yote.

Je umemwangalia mtumishi wangu Ayubu?

"Je umefikiri kuhusu mtumishi wangu Ayubu?" Hapa Mungu alianza kuzungumza na Shetani kuhusu Ayubu. "Angalia mtumishi wangu Ayubu"

mtu mwenye haki na mkamilifu

Neno "mwenye haki" na "mkamilifu" yana maana sawa na yanaeleza kwamba Ayubu alikuwa muadilifu. "Alitenda yaliyo mema mbele za Mungu."

mmoja aliyemcha Mungu na kuepukana na uovu

"mmoja aliyemheshimu Mungu" na "alikataa kufanya uovu." Hapa uovu unazungumziwa kama vile eneo ambalo mtu ataepuka kwenda huko, badala ya kufanya matendo maovu