sw_tn/jas/03/07.md

964 B

Kila aina ya .... na mwanadamu.

Usemi huu "kila aina" humaanisha "aina nyingi." hii inaweza kutafsriwa kama fungu la maneno yanayoonesha kutenda; "Watu wamejifunza kudhibiti aina nyingi za wanyama wa mwitu, ndege, vitambaavyo, na viumbe wa baharini."

Kitambaacho.

Huyu ni mnyama ambaye hutembea juu ya ardhi kwa kujikokota.

Kiumbe wa baharini

Huyu ni mnyama ambaye anaishi majini.

Lakini kuhusu ulimi hakuna hata mmoja miongoni mwa watu awezaye kuchunga ulimi.

Hapa "ulimi" humaanisha kile ambacho mtu hutamka. Maana kamili inaweza kutajwa kwa uwazi kama hivi: "hakuna mtu hata mmoja awezaye kudhibiti ulimi wake pasipo msaada wa Mungu."

Muovu asiyedhibitiwa

Ulimi umezungumziwa kama vile ni uovu usioweza kudhibitiwa. Yakobo anafananisha na tamaa za mtu kuongea mambo maovu.

Umejaa sumu ya kufisha

Yakobo anafananisha uwezo wa mtu kuongea mabaya kama vile nyoka au mmea wenye sumu. Sumu ni maneno yaumizayo ambayo yanaweza kusemwa kwa mtu.