sw_tn/isa/66/12.md

748 B

Maelezo ya Jumla

Yahwe anaendelea kuzungumza juu ya Yerusalemu kana kwamba ilikuwa mama.

kama mto ... kama kijito kinachomwagikia

Hii ina maana Mungu atasababisha watu wa mataifa kuleta kiasi kikubwa cha utajiri, ambacho kitakuwa cha kudumu kama mto na wingi.

Utanyonya kando yake, kubebwa mikononi mwake, na kuchezeshwa juu ya magoti yake

Hii ina maana Yerusalemu itakuwa sehemu ya usalama na faraja kwa watu wa Mungu.

kubebwa mikononi mwake, na kuchezeshwa juu ya magoti yake

Hii inaweza kuelezwa katika hali ya kutenda. "atakubeba mikononi mwake na kukurusha juu ya magoti yake kwa furaha"

kwa hiyo nitakufariji, na utafarijiwa Yerusalemu

Hii inaweza kuelezwa katika hali ya kutenda. "kwa hiyo nitakufariji katika Yerusalemu"