sw_tn/isa/47/06.md

1020 B

Kauli Kiunganishi

Yahwe anaendelea kuzungumza na Babeli kuhusu anguko lake kana kwamba alikuwa malkia ambaye ameaibishwa.

Nilikasirishwa

Hapa "nilikasirishwa" ina maana ya Yahwe.

nilitia unajisi urithi wangu

Yahwe anazungumzia watu wa Israeli kuwa milki yake maalumu kana kwamba walikuwa urithi wake. "Niliwanajisi watu wangu, ambao walikuwa milki yangu maalumu"

kuwakabidhi mikononi mwako

Hapa neno "mkononi" inawakilisha nguvu na utawala wa Babeli. "Ninawaweka chini ya nguvu yako"

umeweka nira nzito sana juu ya watu wazee

Yahwe anazungumzia Wababeli kuwakandamiza watu wazee kana kwamba wamewatendea watu wazee kama ng'ombe na kuweka nira nzito juu ya shingo zao.

nitatawala milele kama malkia wa enzi

Babeli inazungumzia kutawala kwa kudumu juu ya mataifa mengi kana kwamba ilikuwa malkia ambaye atatwala milele.

Hukuviweka vitu hivi moyoni

Yahwe anazungumzia juu ya kufikiria kwa makini kuhusu kitu kana kwamba ilikuwa ni kuweka kitu hicho ndani ya moyo wa mtu. "Haukufikiria vitu hivi"