sw_tn/isa/06/08.md

1.1 KiB

Taarifa ya Jumla

Isaya anaendelea kufafanua ono lake.

sauti ya Bwana inasema

Hapa "sauti" inawakilisha Bwana mwenyewe. "Bwana anasema"

nimtume nani

Inadokezwa ya kwamba Yahwe atamtuma mtu kuzungumza ujumbe wake kwa watu wa Israeli. "Nani nitamtuma kuwa mjumbe kwa watu wangu"

nani ataenda kwa ajili yetu

Inaonekana "yetu" ina maana ya Yahwe na washiriki wa baraza lake la mbinguni.

watu hawa

"watu wa Israeli"

Sikilizeni, lakini msielewe; tazameni, lakini msitambue

Maana zawezekana kuwa 1) vitenzi vya kuamuru "msielewe" na "mstambue" vinaeleza kile Mungu anasababisha kufanyika. "Utasikia, lakini Yahwe hatakuruhusu uelewe; utatazama kwa makini, lakini Yahwe hataruhusu uelewe" au 2) vitenzi vya kuamuru "Sikiliza" na "tazama" zinaeleza wazo la "kama". "Hata kama ukisikiliza hautaelewa; hata kama utatazama kwa makini, hautaelewa"

Sikilizeni, lakini msielewe; tazameni, lakini msitambue

Unaweza kueleza taarifa inayoeleweka kwa uwazi. "Sikiliza ujumbe wa Yahwe, lakini usielewe maana yake; tazama kile Yahwe anachofanya, lakini usigundue maana yake"