sw_tn/isa/01/04.md

962 B

Taarifa ya Jumla

Isaya anazungumza na watu wa Yuda katika mtindo wa shairi.

Taifa, wenye dhambi

Maana zawezekana kuwa 1) Isaya anasema mambo mawili tofauti juu yao. "Taifa la Israeli, nyie wenye dhambi" au 2) anasema jambo moja tu kuhusu wao. "Taifa la wenye dhambi"

watu waliolemewa kwa udhalimu

Kitu kizito sana ambacho mtu anweza kubeba ni sitiari ya dhambi nyingi. "dhambi yao ni kama mfuko mzito juu ya mabega yao unaowafanya vigumu kwao kutembea"

mtoto wa waovu

Neno "mtoto" ni sitiari ya watu ambao hufanya kile wengine walichokwisha fanya. "watu ambao hufanya uovu ule ule wanaouona wengine wakifanya"

tenda mabaya

fanya mambo maovu

Wamemtelekeza Yahwe

"Wameondoka mbali kutoka kwa Yahwe"

wamemdharau

"wamekataa kutii" au "wamekataa kuheshimu"

Israel

Yuda ni sehemu ya iliyokuwa taifa la Israeli.

Wamejitenganisha kutoka kwake

Ingawa katika kipindi kimoja walikuwa marafiki, kwa sasa wanamtendea kana kwamba hawamjui.