forked from WA-Catalog/sw_tn
1001 B
1001 B
Taarifa ya jumla
Nabii Hosea anazungumza.
Utafanya nini siku ya sikukuu iliyowekwa rasmi, siku ya sikukuu ya Yahweh?
Hosea anatumia swali hili kusisitiza kuwa watu hawataweza kushuhudia sikukuu zao ikiwa adui watawashinda na kuwashukua mateka.
siku ya sikukuu iliyowekwa rasmi ... siku ya sikukuu ya Yahweh
Zote hizi zina maana moja.
Kama wamekimbia
Hapa wanazungumziwa wana wa Israeli.
Misri itawakusanya, na Nofu itawazika
Misri na Nofu inamaanisha watu wanaoishi pale. "Jeshi la Wamisri litawakamata, mtakufa huko na watu wa mji wa Nofu watawazika"
Maana hazina zao za pesa- michongoma mikali itakuwa nao
Michongoma imeota sehemu ambayo Israeli walihifadhi fedha zao michongoma hii imefananishwa na adui ambaye atakuja kuchukua mali wanazomiliki Waisraeli.
michongoma itakuwa nao, na miiba itajaza hema zao.
"michongoma" na "miiba" inamaana moja. Michongoma na miiba ikiota inamanisha ardhi hiyo ni kama jangwa.
Hema zao
Hapa "hema" inawakilisha nyumba za Waisraeli.