sw_tn/hos/05/03.md

783 B

Taarifa ya jumla:

Bwana anazungumza kuhusu Israeli.

Najua Efraimu, na Israeli hajajificha kwangu

"Efraimu" na "Israeli" ni watu ambao wanaishi kaskazini mwa ufalme wa Israeli. Hapa Mungu anasema kuwa anawafahamu wao ni akina nani na nini wanafanya.

Efraimu, sasa umekuwa kama kahaba

Efraimu amesimama kama kahaba kwa sababu watu sio waaminifu kwa Mungu kama vile kahaba sio mwaminifu kwa mwanaume mmoja.

maana mawazo ya uzinzi yako ndani yao

Hii inamaanisha kuwa wanatamani kutokuwa waaminifu kwa Mungu. Wanataka kuabudu miungu.

kumgeukia Mungu ... hawatamjua Bwana.

"kunigeukia mimi ... hawakunijua mimi" au "kunigeukia mimi ... hawakunijua mimi, Bwana."

na hawatamjua Bwana

Israeli hawakumtii tena Mungu kwa namna yoyote. Hawakumtambua Bwana kama Mungu wao.