sw_tn/hos/05/01.md

698 B

Sentensi unganishi:

Bwana anazungumza kuhusu Israeli.

Mmekuwa mtego huko Mizpa na wavu uliosambazwa juu ya Tabori.

Mtego na wavu ni vifaa vinavotumika kukatatia mawindo. Misoa na Tabori yalikuwa maeneo ya kuabudia miungu katika nchi ya Israeli.

Waasi husimama sana katika mauaji

"waasi" ni wale wote waliomuasi Bwana na mauaji inaelezea namna ambavyo mauaji ya watu wasio na hatia yanafanyika ikiwemo kutoa kafara kwa miungu ya kipagani.

Waasi

Mtafsiri anaweza kuiweka hii kama "ninyi waasi" kwa sababu Mungu anazungumza juu ya watu waasi wa Israeli.

mauaji

Baadhi ya nakala za kisasa za kiebrania neno hili limesimama kama uovu.

nitawaadhibu wote

"Nitawaadhibu ninyi nyote"