sw_tn/gen/49/28.md

889 B

Haya ni makabila kumi na mbili ya Israeli

"Haya" ina maana ya wana wa Yakobo waliotajwa katika 49:1-27. Kila mwana alikuwa kiongozi wa kabila lake mwenyewe.

alipowabariki

Hapa neno "alipowabariki" lina maana ya kuongelea baraka rasmi.

kila mmoja kwa baraka iliyomstahili

"Akawapa kila mtoto baraka inayomstahili"

akawaelekeza

"akawaamuru"

Ninakaribia kwenda kwa watu wangu

Hii ni njia ya upole ya kusema ya kwamba amekaribia kufa. "Nimekaribia kufa"

kwenda kwa watu wangu

Yakobo ana maanisha pale ambapo nafsi yake utakwenda atakapokufa. Anategemea kuwaunga Abrahamu na Isaka katika maisha ya baadae.

Efroni Mhiti

Hili ni jina la mwanamume. "Mhiti" ina maana ya "uzao wa Hethi".

Makpela

Makpela lilikuwa jina la eneo au mahali.

Mamre

Hili lilikuwa jina lingine la mji wa Hebroni. Inawezekana lilitajwa baada ya Mamre, rafiki wa Abrahamu aliyeishi kule.