forked from WA-Catalog/sw_tn
24 lines
886 B
Markdown
24 lines
886 B
Markdown
# Farao akavua pete yake ya mhuri ... mkufu wa dhahabu shingoni mwake
|
|
|
|
Matendo haya yote yanaashiria ya kwamba Farao anampatia Yusufu mamlaka kufanya kila kitu ambacho Yusufu alipanga.
|
|
|
|
# pete ya mhuri
|
|
|
|
Pete hii ilikuwa na mhuri wa Mfalme uliochongwa juu yake. Hii ilimpatia Yusufu mamlaka na fedha iliyohitajika kutekeleza mipango yake.
|
|
|
|
# mavazi ya kitani safi
|
|
|
|
"Kitani" ni kitambaa kilaini, kigumu kinachotengenezwa na mmea wa kitani.
|
|
|
|
# Akataka apandishwe katika kibandawazi cha pili alichokuwa nacho
|
|
|
|
Tendo hili linadhihirisha wazi kwa watu ya kwamba Yusufu ni wa pili tu kutoka kwa Farao.
|
|
|
|
# Pigeni magoti
|
|
|
|
"Inama chini na mheshimu Yusufu". Kupiga goti na kuinama chini ilikuwa ishara ya heshima na taadhima.
|
|
|
|
# Farao akamweka juu ya nchi yote
|
|
|
|
Msemo "kukuweka juu" una maana ya kumpatia mamlaka. Hapa "nchi" ina maana ya watu. "Nimekupa mamlaka juu ya kila mmoja ndani ya Misri"
|