sw_tn/gen/41/42.md

886 B

Farao akavua pete yake ya mhuri ... mkufu wa dhahabu shingoni mwake

Matendo haya yote yanaashiria ya kwamba Farao anampatia Yusufu mamlaka kufanya kila kitu ambacho Yusufu alipanga.

pete ya mhuri

Pete hii ilikuwa na mhuri wa Mfalme uliochongwa juu yake. Hii ilimpatia Yusufu mamlaka na fedha iliyohitajika kutekeleza mipango yake.

mavazi ya kitani safi

"Kitani" ni kitambaa kilaini, kigumu kinachotengenezwa na mmea wa kitani.

Akataka apandishwe katika kibandawazi cha pili alichokuwa nacho

Tendo hili linadhihirisha wazi kwa watu ya kwamba Yusufu ni wa pili tu kutoka kwa Farao.

Pigeni magoti

"Inama chini na mheshimu Yusufu". Kupiga goti na kuinama chini ilikuwa ishara ya heshima na taadhima.

Farao akamweka juu ya nchi yote

Msemo "kukuweka juu" una maana ya kumpatia mamlaka. Hapa "nchi" ina maana ya watu. "Nimekupa mamlaka juu ya kila mmoja ndani ya Misri"