sw_tn/gen/39/21.md

949 B

Lakini Yahwe alikuwa pamoja na Yusufu

Hii ina maana ya namna Yahwe alivyomtunza Yusufu na kuwa mema kwake. "Lakini Yahwe alikuwa mwema kwa Yusufu" au "Lakini Yahwe alimtunza Yusufu"

Akampa kibali mbele ya mlinzi wa gereza

Hii ina maana Yahwe alisababisha mlinzi wa gereza kumkubali Yusufu na kumtendea wema. "Yahwe alisababisha mlinzi wa gereza kufurahishwa na Yusufu"

mlinzi wa gereza

"msimamizi wa gereza" au "mtu mwenye usamamizi na gereza"

akawaweka mikononi mwa Yusufu

Hapa "mkononi" unawakilisha nguvu ya Yusufu au uaminifu. "kumweka Yusufu juu ya"

Chochote walichokifanya, kilikuwa chini ya uangalizi wa Yusufu

"Yusufu alikuwa mwanaglizi wa kila kitu walichofanya pale"

kwa sababu Yahwe alikuwa pamoja naye

Hii ina maana ya jinsi Yahwe alivyomsaidia Yusufu na kumuongoza. "kwa sababu Yahwe alimuongoza Yusufu"

Yahwe akafanikisha kila alichokifanya.

"Yahwe alisababisha kila kitu ambacho Yusufu alifanya kufanikiwa"