sw_tn/gen/34/27.md

643 B

maiti

"maiti ya Hamori, Shekemu na wanamume wao"

pora mji

"waliiba kila kitu chenye thamani katika mji ule"

kwa sababu watu wale walikuwa wamemnajisi dada yao

Shekemu pekee alimnajisi Dina, lakini wana wa Yakobo walichukulia familia yote ya Shekemu na kila mtu katika mji kuhusika na tendo hili.

walikuwa wamemnajisi

Hii ina maana ya kwamba Shekemu alimvunjia heshima na kumuabisha sana Dina kwa kumlazimisha kulala naye.

Wakachukua makundi yao

"wana wa Yakobo wakachukua mifugo ya watu wale"

utajiri wao wote

"mali zao zote na fedha"

Watoto na wake zao wote, wakawachukua

"Waliwakamata watoto wao na wake zao wote"