sw_tn/gen/34/11.md

773 B

Shekemu akamwambia baba yake

"Shekemu alimwambia baba yake Dina Yakobo"

Na nione kibari machoni penu, na chochote mtakachoniambia nitatoa

Hapa "machoni" ina maana ya fikra na mawazo ya mtu. "Kama utanipa kibali, basi nitakupa chochote utakachokiomba"

mahari

Katika baadhi ya tamaduni, ni kawaida kwa mwanamume kutoa fedha, mali, ng'ombe, na zawadi zingine kwa familia ya mwanamke katika kipindi cha ndoa.

Wana wa Yakobo wakamjibu Shekemu na Hamori baba yake kwa hila

Nomino inayojitegemea ya "hila" inaweza kuwekwa kama kitenzi cha "kudanganya". "Lakini wana wa Yakobo walimdanganya Shekemu na Hamori walipowajibu"

Shekemu alikuwa amemnajisi Dina

Hii ina maana ya kwamba Shekemu aliwavunjia heshima sana na kumuabisha Dina kwa kumlazimisha kulala naye.