sw_tn/gen/01/14.md

1.5 KiB

Kuwe na mianga katika anga

Hii ni amri. Kwa kuamuru ya kwamba mianga iwepo, Mungu alifanya iwepo

mianga katika anga

"vitu ving'aavyo katika anga" au"vitu vitoavyo mwanga katika anga". Hii inaamanisha jua, mwezi na nyota

katika anga

"katika uwazi wa anga" au "katika uwazi mkubwa wa anga"

kutenganisha mchana na usiku

"kutenganisha mchana na usiku." Hii inamaanisha "kutusaidia kutambua tofauti kati ya mchana na usiku." Jua inamaanisha ni mchana, na mwezi na nyota humaanisha ni usiku.

na ziwe kama ishara

Hii ni amri. Kwa kuamuru ya kwamba ziwe kama ishara, Mungu alizifanya zitumike kama ishara. "Na zitumike kama ishara" au "na zioneshe"

ishara

Hapa inamaanisha kitu kinachofunua au kinacholenga jambo

majira

"Majira" inamaanisha nyakati zitakazotengwa kwa sikukuu na mambo mengine ambayo watu hufanya.

kwa majira, kwa siku na miaka

Jua, mwezi, na nyota huonyesha muendelezo wa muda. Hii inatusaidia kutambua ni wakati gani tukio hutokea kila wiki, mwezi au mwaka.

ziwe mianga katika anga ili kutoa mwanga juu ya nchi

Hii ni amri. Kwa kuamuru ziwe mianga juu ya nchi, Mungu alifanya zimulike juu ya nchi

kutoa mwanga juu ya nchi

"kutoa mwanga juu ya nchi" au "kuangazia nchi". Nchi haitoi mwanga yenyewe bali hupata mwanga na kurudisha mwanga.

ikawa hivyo

"ilitokea kama hivyo" au "Hivyo ndivyo ilivyotokea". Mungu alichoamuru kilitokea kama alivyotamka kitokee. Msemo huu hujitokeza katika sura nzima na una maana ile ile kila unapojitokeza.