sw_tn/gen/01/03.md

698 B

Na kuwe na nuru

Hii ni amri. Kwa kuamuru kuwepo na nuru, Mungu alifanya iwepo.

Mungu akaona nuru, kuwa ni njema

"Mungu aliifikiria nuru na kufurahishwa nayo." Hapa "Njema" inamaanisha "kufurahisha" au "inayofaa."

akaigawa nuru na giza

"alitenganisha nuru na giza" au "alifanya kuwepo na nuru wakati mmoja na giza wakati mwingine." Hii inamaanisha Mungu aliumba wakati wa mchana na usiku.

Ikawa jioni na asubuhi, siku ya kwanza

Mungu alifanya vitu hivi katika siku ya kwanza ambapo ulimwengu ulianza kuwepo.

jioni na asubuhi

Hii inamaanisha siku nzima. Mwandishi anazungumzia siku nzima kana kwamba ni sehemu mbili. Kwa tamaduni za Kiyahudi, siku moja huanza baada ya jua kuzama.