sw_tn/ecc/01/12.md

680 B

Nilitia akili yangu

"Nikusudia" au "Niliamua"

kusoma na kutafuta

Misemo hii miwili inamaanisha kitu kimoja na inasisitiza alisoma kwa bidii.

wana wa watu

"binadamu"

matendo yote ambayo yanafanyika

"kila kitu ambacho watu hufanya"

mvuke

"umande" au "pumzi." Haidumu. "cha muda" au "haina maana." Kile ambacho watu wanafanya ni kama umande kwa sababu hakidumu na hakina maana.

kujaribu kuuchunga upepo

Mwalimu anasema kwamba vitu ambavyo watu hufanya ni kama kujaribu kuushika upepo au kuuzuia upepo kupuliza.

Palipopinda hapawezi kunyoshwa! Kisicho kuwepo hakiwezi kuhesabiwa!

"watu hawawezi kunyosha vitu vilivyopinda! Hawawezi kuhesabu kisichokuwepo!"