sw_tn/act/18/24.md

1.2 KiB

Sentensi unganishi

Luka anaelezea kile kilichotokea katika Mji wa Efeso wakiwa na Prisila na Akwira

Taarifa ya Jumla

Apolo anatambulishwa kwenye hadithi. Mistari ya 24 na 25 inatoa habari kumuhusu yeye.

Mmoja wa Wayahudi aitwaye Apolo

Hapa Luka anaanza kuelezea habari ya mtu mpya.

Mzaliwa wa Alexandra

"Mtu ambaye alizaliwa katika mji wa Alexandria". Hii inaweza kuwa ni miji ya 1) "Alexandria huko Misiri katika mwambao wa kaskasini. " au 2) Alexandra huko Asia katika mwambao wa magharibi."

ufasaha katika kuongea

"mwongeaji mzuri"

mwenye uwezo katika maandiko

"Alikuwa anayafahamu vema maandiko. Alikuwa anauelewa mzuri wa maandiko ya Agano la Kale.

Apolo alikuwa ameelimishwa vema katika mafundisho ya Bwana.

"Baadhi ya waumini walikuwa wamemfundisha Apolo namna Bwana Yesu alivyokuwa anataka watu wapate kuishi.

Alikuwa na bidii katika roho

Neno "roho" linamtambulisha Apolo kama mtu aliyekuwa mwenye nia thabiti ya roho.

ubatizo wa Yohana

"Ubatizo ambao Yohana alifanya" Huu ni ulinganisho wa ubatizo wa Yohana ambao ulikuwa wa maji na ubatizo wa Yesu ambao ulikuwa wa Roho Mtakatifu.

njia za Mungu

Namna vile anawataka watu waishi.

kwa usahihi

"kwa undani zaidi "