sw_tn/act/14/14.md

933 B

mitume, Barnaba na Paulo

Inawezekana Luka anatumia "mtume" katika hali ya ujumla ya "yule ambaye ametumwa."

walichana nguo zao

Hili ni tendo la ishara kuonesha kuwa walihuzunishwa na kukasirishwa kwamba kundi lilitaka kuwatolea wao sadaka.

Watu, kwa nini mnafanya hivi vitu?

Barnaba na Paulo wanawakaripia watu kwa kujaribu kuwatolea sadaka. "watu, hampaswi kutuabudu!"

Sisi pia ni binadamu wenye hisia kama nyie

Kwa kauli hii, Baranaba na Paulo wanasema kuwa wao sio miungu. "Sisi ni binadamu tu kama nyie.. Sisi sio miungu!"

wenye hisia sawa na nyie

"kama nyie kwa kila hali"

mgeukieni Mungu aliye hai kutoka kwa vitu hivi visivyo na maana

"acheni kuabudu miungu ambayo haiwezi kuwasaidia, na badala yake anzeni kumuabudu Mungu aliye hai"

Mungu aliye hai

"Mungu ambaye kweli yupo" au "Mungu anayeishi"

Siku za nyuma

"katika nyakati za zamani" au "Hadi sasa"

kutembea katika

"kuishi kulingana na"