sw_tn/act/12/13.md

1.2 KiB

Maelezo ya jumla

Maelezo haya yanawataja binti Rhoda pamoja na wote waliokuwa wakiomba mle chumbani.

Alibisha mlangoni

"Petro alibisha mlangoni" Alizidi kugongagonga kama ilivyokuwa desturi ya Wayahudi ili kuruhusu waliopo kujua kuwa wametembelewa.

kwenye mlango wa kizuizi

"Katika mlango wa nje" au "Katika mlango wa kuingilia kutoka barabarani hadi kwenye yadi ya nyumba"

Akaja kufungua

"Alikuja getini kuuliza ni nani aliyekuwa anabisha hodi"

Kwa furaha

"Kwa vile alijawa na furaha" au "Furaha kupita kiasi"

Alishindwa kuufungua mlango

"Hakuweza kuufungua mlango" au "Alisahau kufungua mlango"

akakimbia ndani ya chumba

"Alikwenda mbio kwenye chumba cha nyumba ile"

na kuwajulisha

liwajulisha au "Alisema"

Petro amesimama mbele ya Mlango

"Amesimama nje mbele ya mlango"

Wewe ni mwendawazimu

Watu siyo tu hawakumwamini, bali walimkemea pia kwa kusema maneno ya kipuuzi.

lakini alikazia kuwa ni kweli

"Alisisitiza kusema alichowaambia kilikuwa cha kweli"

Wakamwambia

"Walimwambia"

Ni malaika wake

"KIle ulichokiona ni malaika wa Petro" Wayahudi waliamini kuwa na malaika mlinzi na inawezekana walifikiri kwa Petro hivyo, kuwa malaika wa Petro alikuwa amekuja kwao.