forked from WA-Catalog/sw_tn
983 B
983 B
kwamba Israeli wote wakusanywe pamoja kwako
Askari wote wanatajwa hapa kama "Israeli wote"
kutoka Dani hadi Beersheba
Kifungu hiki kinamaanisha kutoka mpaka wa kaskazini hadi mpaka wa kusini wa Israeli
wengi kama mchanga ulioko ufuweni mwa bahari
Hii ni kuzidisha maana pale chembe zote za mchanga zinalinganishwa na idadi ya askari wa Israeli.
kwamba wewe mwenyewe unakwenda vitani
Kifungu hiki "binafsi" kinamaanisha kwenda wewe mwenyewe na wala siyo kutuma mtu mwingine.
kuja juu yake
Hii inamaana ya kwenda kwake kwa kusudi la kumshambulia.
tutamfunika kama umande unavyofunika ardhi
Jeshi la Absalomu linaelezwa kulifunika jeshi la Daudi kama umande unavyoifunika ardhi wakati wa asubuhi.
umande
mvuke unaoanguka juu ya ardhi kama maji na kuifunika ardhi wakati wa usiku na kuacha ardhi imeloa.
Hatutaacha hata mmojawao ... akiwa hai
Sentensi hii imetumika kusisitiza kwamba watamwua kila mtu.
Yeye mwenyewe
Maneno haya yote yanamtaja Daudi.