sw_tn/2sa/17/11.md

983 B

kwamba Israeli wote wakusanywe pamoja kwako

Askari wote wanatajwa hapa kama "Israeli wote"

kutoka Dani hadi Beersheba

Kifungu hiki kinamaanisha kutoka mpaka wa kaskazini hadi mpaka wa kusini wa Israeli

wengi kama mchanga ulioko ufuweni mwa bahari

Hii ni kuzidisha maana pale chembe zote za mchanga zinalinganishwa na idadi ya askari wa Israeli.

kwamba wewe mwenyewe unakwenda vitani

Kifungu hiki "binafsi" kinamaanisha kwenda wewe mwenyewe na wala siyo kutuma mtu mwingine.

kuja juu yake

Hii inamaana ya kwenda kwake kwa kusudi la kumshambulia.

tutamfunika kama umande unavyofunika ardhi

Jeshi la Absalomu linaelezwa kulifunika jeshi la Daudi kama umande unavyoifunika ardhi wakati wa asubuhi.

umande

mvuke unaoanguka juu ya ardhi kama maji na kuifunika ardhi wakati wa usiku na kuacha ardhi imeloa.

Hatutaacha hata mmojawao ... akiwa hai

Sentensi hii imetumika kusisitiza kwamba watamwua kila mtu.

Yeye mwenyewe

Maneno haya yote yanamtaja Daudi.