sw_tn/2sa/12/09.md

763 B

Hivyo kwa nini umedharau... Yahwe, hata kufanya maovu mbele zake?

Swali hili linatumika kumkemea Daudi. Yaani "haukupaswa kumdharau ... Yahwe na kufanya yaliyomaovu mbele zake!"

Hata kufanya yaliyomaovu mbele zake

"Mbele" ya Yahwe inarejea kwa kile anachofikiri. Hii inazungumzia anachohesabu kuwa uovu halisi.

Umemwua Uria Mhiti kwa upanga

Daudi hakumwua Uria kwa mkono wake, bali alipanga Uria alivyouawa. Kifungu "kwa upanga" kinaonesha jinsi alivyokufa vitani.

Ulimwua kwa upanga wa jeshi la Amoni

Inaonesha kwamba Daudi hakumwua kwa mkono wake bali alipanga jinsi ya kuuawa kwa Uria mkononi mwa Waamoni.

Upanga hautaondoka nyumbani mwako

Hapa neno "upanga" linaonesha watu wanaokufa vitani. "Nyumba" ya Daudi inarejerea wazawa wake.