sw_tn/2jn/01/01.md

1.2 KiB

Sentensi Unganishi

Baada ya salamu, Yohana anawaonyesha waumini kuwa upendo na kweli vinakwenda sambamba

Maelezo ya Jumla

Kihistoria mtume Yohana amekubalika kuwa ndiye mwandishi wa barua hii. Anasema "pendaneni" hii pengine barua hii liliandikiwa kanisa.

Maelezo ya Jumla

"ninyi" na "yenu" katika barua hii yanaonyesha wingi

Maelezo ya Jumla

katika barua hii Yohana anatumia maneno "sisi" na 'yetu" ikimaanisha Yohana mwenyewe pamoja na wasomaji wake

Kutoka kwa mzee kwenda kwa mwanamke mteule na watoto wake

Barua za wakati huo zilianza na jina la mwandishi, kwa kushupisha inaweza kusomeka:- " mimi, Yohana mzee, ninaandika barua hii kwa mwanamke mteule na watoto wake"

Mzee

Ni rejea kwa Yohana, mtume na mwanafunzi wa Yesu. Anajiita mzee labda kwa sababu ya umri wake mkubwa au kwa sababu ni kiongozi kanisani.

kwa mwanamke mteule na watoto wake

Pengine hii ina maana ya kundi au kusanyiko na waumini .

ambaye nampenda katika kweli.

" Ninyi watu ninaowapenda katika kweli"

wanao ifahamu kweli

"ambao wanao fahamu ukweli kuhusu Mungu na Yesu"

Baba...Mwana

Hivi ni vyeo muhimu vinavyoelezea uhusiano kati ya Mungu na Yesu

katika kweli na upendo.

Neno "kweli" linaelezea "upendo." Pengine inamaanisha "katika upendo wa kweli"