Baadhi ya tafsiri hupendelea kuweka kando kidogo nukuu za Agano la Kale. ULB na tafsiri nyingine nyingi za Kiingereza huingiza mstari yote ya mistari ya 6 na18, ambayo ni nukuu kutoka Agano la Kale.
Tafsiri za Kiingereza hutumia maneno mengi tofauti ili kutafsiri maneno haya. Maneno haya ni pamoja na "wanajimu" na "watu wenye hekima." Watu hawa wangeweza kuwa wanasayansi au majusi. Ni bora kutafsiri hii kwa neno la kawaida "waakili," inapowezekana.