Luka katika sura hii anatumia maelezo mengi ili kuonyesha ufufuo wa Yesu kutoka kwa wafu. Luka anaonyesha kwamba haikuwezekana kwa mtu mwingine kufa kwa niaba ya Yesu. Anaonyesha pia kwamba ufufuo haukuwa mfano. (See: [[rc://*/tw/dict/bible/kt/resurrection]] and [[rc://*/ta/man/translate/figs-metaphor]])
Inasemekana kuwa Yesu alifufuka kutoka wafu siku ya tatu. Alikufa siku ya Ijumaa alasiri (kabla ya kutua kwa jua) na kufufuliwa Jumapili. Katika Israeli ya kale, siku ilianza na kumalizika wakati wa kutua kwa jua. Pia walihesabu sehemu yoyote ya siku kama "siku."
Mathayo, Marko, Luka, na Yohana wote waliandika juu ya malaika waliovalia nguo nyeupe wakiwa pamoja na wanawake katika kaburi la Yesu. Waandishi wawili kati yao waliwaita wanaume, lakini ni kwa sababu tu malaika walikuwa katika hali ya kibinadamu. Waandishi wawili waliandika kuhusu malaika wawili, lakini waandishi wengine wawili waliandika juu ya moja tu. Ni bora kutafsiri kila moja ya vifungu hivi kama inavyoonekana katika ULB bila kujaribu kufanya vifungu vyote kufanana. (Angalia: Mathayo 28:1-2, Marko 16: 5 na Luka 24: 4 na Yohana 20:12)