sw_tn/luk/17/20.md

20 lines
724 B
Markdown
Raw Permalink Normal View History

2018-04-12 01:01:04 +00:00
# Habari kwa ujumla:
Hii ni sehemu ya pili ya hadithi. Hatujui ambapo hili limetokea; ni siku moja wakati Yesu akizungumza na Mafarisayo.
# Alipoulizwa na mafarisayo ufalme wa Mungu utakuja lini, Yesu akawajibu akisema,
Hii inaweza semwa kama: "wakamuuliza 'Lini Utawala wa Mungu utakuja?"
# Alipoulizwa na Mafarisayo
Huu ni mwanzo wa sehemu mpya ya hadithi. Baadhi ya tafsiri huanza kwa "Siku moja" au "Mara."
# Ufalme wa Mungu sio kitu ambacho kinaweza kuonekana
Hii inaweza kusemwa: "Ufalme wa Mungu si kitu ambacho unaweza kuona kwa macho yako" au "Ingawa unanngalia Ufalme wa Mungu, huwezi kuuona"
# Utawala wa Mungu uko kati yenu
"Utawala wa Mungu uko hapa" au "Mungu tayari ameanza kutawala kati yenu"