sw_tn/gen/40/20.md

930 B

Ikawa

"Hapo baadae, katika siku ya tatu". msemo "ikawa" unatumika hapa kuweka alama kwa tukio jipya katika simulizi.

Akafanya sherehe

"Akawa na sherehe"

mkuu wa wanyweshaji

Huyu alikuwa mtu kiongozi ambaye aliandaa na kuhudumia vinywaji kwa mfalme.

mkuu wa waokaji

Huyu alikuwa mtu kiongozi ambaye aliandaa chakula kwa ajili ya mfalme.

Akamrudisha mkuu wa wanyweshaji katika majukumu yake

"majukumu" wa mkuu wa wanyweshaji una maana ya kazi yake kama mkuu wa manyweshaji. "Alimrudishia mkuu wa wanyweshaji kazi yake"

Lakini akamtundika mkuu wa waokaji

Farao hakumnyonga mwokaji yeye binafsi, ila aliaamuru anyongwe. "Lakini aliamuru mkuu wa waokaji anyongwe" au "Lakini aliamuru walinzi wake kumnyonga mkuu wa waokaji"

kama Yusufu alivyokuwa amewatafsiria

Hii ina maana ya pale ambapo Yusufu alitafsiri ndoto zao. "kama vile Yusufu alivyosema kingetokea pale alipotafsiri ndoto za wanamume wale wawili"