1.3 KiB
Taarifa ya Jumla:
Usambamba ni kawaida katika mashairi ya Kiebrania.
Kwa mwanamuziki mkuu
"Hii ni kwa kiongozi wa muziki kutumia katika kuabudu"
weka katika Al Tashhethi
Hii inawezakuwa inaeleza mtindo wa muziki au tuni ya kutumia wakati wa kuimba zaburi hii. "imba zaburi hii kwa kutumia tuni ya 'Al Tashhethi'" au
Al Tashhethi
Hii inamaanisha "Usiangamize."
Zaburi ya Daudi
Maana zinazowezekana ni 1) Daudi aliiandika zaburi au 2) zaburi inamhusu Daudi au 3) zaburi iko katika mtindo wa zaburi za Daudi.
Michtamu
Maana ya neno "michtamu" haiko wazi. Hii inaweza kuandikwa kama: "Hii ni zaburi aliyoandika Daudi."
alipotoroka kutoka kwa Sauli, katika pango
"Hii ina husu Daudi alipojificha kwenye pango akimkimbia Sauli" au "Hii ina husu wakati mfalme Sauli alipokuwa anamfukuza Daudi, na Daudi akajificha kwenye pango"
ninakukimbilia
Kwenda kwa Yahwe kwa ajili ya ulinzi inazungumziwa kama kumkimbilia. "ninaenda kwako kwa ajili ya ulinzi"
ninakaa chini ya mbawa zako kwa ajili ya ulinzi
Mwandishi anamzungumzia Mungu kana kwamba ni ndege anayelinda makinda yake kwa kuwaficha chini ya mbawa zake. "nakuamini wewe kunilinda"
hadi uharibifu wake uishe
Mwandishi wa zaburi anazungumzia hamu ya Sauli kumuua kana kwamba Sauli alikuwa akitafuta kumwangamiza adui. "hadi shida hii iishe" au "hadi nitakapo kuwa siko hatarini tena"