sw_tn/psa/057/001.md

1.3 KiB

Taarifa ya Jumla:

Usambamba ni kawaida katika mashairi ya Kiebrania.

Kwa mwanamuziki mkuu

"Hii ni kwa kiongozi wa muziki kutumia katika kuabudu"

weka katika Al Tashhethi

Hii inawezakuwa inaeleza mtindo wa muziki au tuni ya kutumia wakati wa kuimba zaburi hii. "imba zaburi hii kwa kutumia tuni ya 'Al Tashhethi'" au

Al Tashhethi

Hii inamaanisha "Usiangamize."

Zaburi ya Daudi

Maana zinazowezekana ni 1) Daudi aliiandika zaburi au 2) zaburi inamhusu Daudi au 3) zaburi iko katika mtindo wa zaburi za Daudi.

Michtamu

Maana ya neno "michtamu" haiko wazi. Hii inaweza kuandikwa kama: "Hii ni zaburi aliyoandika Daudi."

alipotoroka kutoka kwa Sauli, katika pango

"Hii ina husu Daudi alipojificha kwenye pango akimkimbia Sauli" au "Hii ina husu wakati mfalme Sauli alipokuwa anamfukuza Daudi, na Daudi akajificha kwenye pango"

ninakukimbilia

Kwenda kwa Yahwe kwa ajili ya ulinzi inazungumziwa kama kumkimbilia. "ninaenda kwako kwa ajili ya ulinzi"

ninakaa chini ya mbawa zako kwa ajili ya ulinzi

Mwandishi anamzungumzia Mungu kana kwamba ni ndege anayelinda makinda yake kwa kuwaficha chini ya mbawa zake. "nakuamini wewe kunilinda"

hadi uharibifu wake uishe

Mwandishi wa zaburi anazungumzia hamu ya Sauli kumuua kana kwamba Sauli alikuwa akitafuta kumwangamiza adui. "hadi shida hii iishe" au "hadi nitakapo kuwa siko hatarini tena"