sw_tn/psa/049/014.md

1.2 KiB

Taarifa ya jumla:

Mwandishi anaendelea kuwaelezea watu wanaoamini kuwa mali yao itawaokoa.

Kama kondoo

Mwandishi anawafananisha watu watakaokufa kama kundi la kondoo. Kama kondoo amabvyo hawawezi kutoroka wakati bucha anapoamua kuwachinja, kwa hiyo watu hawatatoroka ukifika wakati wao kufa.

wamechaguliwa

"Mungu amewachagulia"

mauti itakuwa mchungaji wao

Mwandishi anazungumzia watu kufa kwa kutaja mauti kama mtu ambaye ni mchungaji anayewaongoza katika kaburi. "mauti itawapeleka kama mchungaji anavyowaongoza kondoo kwenda machinjioni"

asubuhi

Hapa neno "asubuhi" ni sitiari inayomaanisha wakati ambapo Mungu atawathibitisha watu wenye haki na kuwaokoa kutoka kwa watu waovu.

miili yao itamezwa kuzimu

Mwandishi anazungumzia kuzimu, sehemu ya wafu, kana kwamba ni mtu au mnyama. Anazungumzia uozo wa miili iliyokufa kana kwamba kuzimu inaila. "miili yao itaoza kaburini"

Mungu atakomboa maisha yangu kutoka kwenye nguvu ya kuzima

Mwandishi anazungumzia kuzimu kana kwamba ni mtu aliye na nguvu juu ya wale walio kufa. Kutokana na muktadha, inadokezwa kwamba uwezo huu unamaanisha kuteketeza miili ya wafu.

Mungu atakomboa maisha yangu

Hapa neno "maisha" linamaanisha mtu mzima. "Mungu atanikomboa"