sw_tn/psa/048/001.md

1.2 KiB

Taarifa ya Jumla:

Huu ni wimbo kuhusu Yerusalemu kuwa sehemu ya kuishi ya Mungu.

Taarifa ya Jumla:

Usambamba ni kawaida katika mashairi ya Kiebrania.

zaburi ya wana Kora

"hii ni zaburi ambayo wana wa Kora waliandika"

mwenye kusifiwa sana

"watu wanapaswa kumsifu sana"

mji wa Mungu wetu katika mlima wake mtakatifu

Hii inamaanisha Yerusalemu, iliyojengwa katika mlima Sayuni.

mji wa Mungu wetu

Maana zinazowezekana ni 1) "mji ambao Mungu wetu huishi" au 2) "mji ulio wa Mungu wetu"

Mzuri katika kuinuka

"Mzuri na juu." Neno "kuinuka" linamaanisha jinsi mlima Sayuni ulivyo juu.

furaha ya dunia yote, ni mlima Sayuni

Hapa neno "dunia" linamaanisha kila mtu anayeishi duniani. "Mlima Sayuni huwapa watu wote duniani furaha" au "watu wote wanafurahi kwa sababu ya mlima Sayuni"

katika pande za kaskazini

Maana zinazowezekana ni kwamba msemo huu 1) unamaanisha mwelekeo wa kaskazini au 2) ni jina jingine la mlima sayuni linalomaanisha "mlima wa Mungu."

Mungu amejifanya kujulikana katika majumba yake kama sehemu ya kukimbilia

Mwandishi anamzungumzia Mungu kana kwamba ni sehemu ambapo watu wanaweza kwenda kwa ajili ya usalama. "Mungu amejifanya kujulikana kama yule anayetoa usalama kwa watu katika majumba ya mlima Sayuni"