forked from WA-Catalog/sw_tn
902 B
902 B
Taarifa ya Jumla:
Hapa ni mwanzo wa maono mengine. Yohana anaanza kuelezea mpandaji wa farasi nyeupe.
Kisha niliona mbingu zimefunguka
Hii picha inatumika kuashiria mwanzo wa maono mapya.
yule aliyekuwa amempanda
Aliyempanda ni Yesu.
Huhukumu kwa haki
Hapa "haki" inamaanisha kile kilicho sahihi. "Anahukumu watu wote kulingana na kile kilicho sahihi"
Macho yake ni kama mwali wa moto
Yohana anazungumzia macho ya mpandaji kama vile yaling'aa kama mwali wa moto.
jina lililoandikwa juu yake
Hii inaweza kuelezwa kwa hali ya kutenda. "Mtu ameandika jina juu yake"
asilolifahamu mtu yeyote isipokuwa yeye mwenyewe
"Yeye tu ndiye ajuae maana ya jina hilo"
Amevaa vazi lililochovywa katika damu
Hii inaweza kuelezwa kwa hali ya kutenda. "Damu imefunika vazi lake"
jina lake anaitwa Neno la Mungu
Unaweza kueleza hii kwa hali ya kutenda. "jina lake pia ni Neno la Mungu"