forked from WA-Catalog/sw_tn
648 B
648 B
kuwa mkweli na utubu
"kuwa makini na utubu"
nasimama katika mlango na kubisha
Yesu anazungumzia watu kutaka kuhusiana naye kama vile wanataka kumkaribisha nyumbani mwao. "Mimi ni kama yule asimamaye mlangoni akibisha hodi"
na kubisha
Watu hubisha hodi wakitaka kukaribishwa kwenye nyumba ya mtu. "na ninataka mniruhusu niingie ndani"
asikiaye sauti yangu
Msemo wa "sauti yangu" huonesha Yesu akizungumza. "anayesikia nikizungumza" au "anayesikia nikiita"
nitakuja na kuingia nyumbani kwake
Lugha zingine zinaweza kupendelea kitenzi cha "nenda". "Nitaenda nyumbani kwake"
na kula naye
Hii huonesha kuwa pamoja kama marafiki.