1.2 KiB
Taarifa ya Jumla:
Usambamba ni kawaida katika mashairi ya Kiebrania.
Zaburi ya Daudi
Maana zinazowezekana ni 1) Daudi aliiandika zaburi au 2) zaburi inamhusu Daudi au 3) zaburi iko katika mtindo wa zaburi za Daudi.
mwamba wangu
Maana zinazowezekana ni1) "yule ambaye ananiweka salama" au 2) "yule anayenipa nguvu"
anayefunza mikono yangu kwa ajili ya vita na vidole vyangu kwa mapambano
Maneno "mikono" na "vidole" zinamaana ya "mimi." "anayeniandaa kwa ajili ya vita" au ""anayeniandaa kwa ajili ya mapambano"
uaminifu wangu wa agano
"yule ambaye ananionesha uaminifu wa agano"
ngome yangu ... namkimbilia
Mwandishi wa zaburi anatumia sitiari kusisitiza kwamba Yahwe atamlinda.
mnara wangu wa juu
Daudi anamzungumzia Yahwe kana kwamba ni ngome inayomlinda dhidi ya mashambulizi. Yahwe ndiye anayemlinda Daudi na hatari.
ngao yangu
Daudi anamzungumzia Yahwe kana kwamba ni ngao inayomlinda askari. Yahwe ndiye anayemlinda Daudi dhidi ya hatari.
yule ambaye namkimbilia
Kwenda kwa Yahwe kunazungumziwa kama kumkimbilia. "yule ambaye ninaenda kwake kwa ajili ya ulinzi"
yule unayedhibiti mataifa chini yangu
"yule anayenisaidia kuyashinda mataifa mengine"