forked from WA-Catalog/sw_tn
569 B
569 B
Macho yangu yanachoka ninaposubiri
Hapa "macho" yanawakilisha mtu mzima. "Ninachoka kwa sababu ninasubiri na kusubiri"
kwa wokovu wako na kwa neno lako la haki
"ili uniokoe kama ulivyoahidi kufanya"
neno lako la haki
Hapa "neno" linawakilisha kile ambacho Mungu anawasiliana na watu. "ahadi yako ya haki"
Mwoneshe mtumishi wako
Mwandishi anajizungumzia mwenyewe kama "mtumishi wako." "Nioneshe" au "Nioneshe mimi, mtumishi wako"
uaminifu wako wa agano
"kwamba unanipenda kwa uaminifu" au "kwa kuwa wewe ni mwaminifu kwangu kwa sababu ya agano lako"